_MG_1256
Wema Sepetu (katikati), Idris Sultan upande wa kulia na kushoto ni Mh. Mbunge wa bunge la Afrika Mashariki, Shy-Rose Bhanji wakipata picha ya pamoja katika jukwaa hilo la kulia ambalo lilikuwa maalum kwa wageni mbalimbali waalikwa na watu maalufu ndani na nje leo wakati wa tukio la kuapichwa kwa Rais wa awamu ya tano, Dk. John Pombe Magufuli. 

Na Andrew Chale, Modewjiblog
[TEMEKE-DAR ES SALAAM] Wakati Watanzania na dunia nzima leo Novemba 5, 2015)  imeshuhudia kuapishwa kwa Rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli,  Mastaa wanaotikisa Bongo na wanapenda kufuatanafuatana kama kumbikumbi, Staa na mrembo, Wema Sepetu ‘Madam’ na mshindi wa Shindano la Big Brother Hotshots 2014, Idris Sultan wametokea kuwa kivutio baada ya uwapo wao katika shughuli hiyo ya kihistoria ndani ya uwanja wa shamba la Bibi.
Modewji blog iliwashuhudia mastaa hao tokea waliposhuka kwenye gari na kisha kuingia kwenye viunga vya uwanja huo wa Bibi, Wakati wa kuwasili kwa wawili hao hali ya mvua ilikuwa ndio inataka kuanza hata hivyo walifika uwanjani na kukuta uwanja umejaa sehemu za wageni waalikwa na kutulia kwa mvua pembeni kabla ya kupatiwa nafasi ya kuketi.
Kwa mujibu wa watu waliokuwa karibu na mtandao huu walinong’oneza kuwa, Wawili hao licha ya kuonekana kuwa nadhifu na umaarufu wao, lakini wameweza kukaa na kujichanganya na watu wengine wa kawaida na kuendelea na shangwe za kumpongeza Dk. Magufuli.
Hata hivyo, kadri ya uwepo wao huo kwenye jukwaa hilo la kulia linalotazama uwanja, wakati walipoingia kukaa, walipata shangwe kubwa ya kushangiliwa na umati mkubwa wa watu huku wengine nao wakishangilia pasipojua wanashangilia nini.. hali hii iliweza kukusanya watu wengi zaidi kwenye jukwaa hilo huku wengi wao wakifika kwa lengo la kuwashuhudia kwa macho huku wengine wakipiga ‘Selfies’ za mbali ilimradi kuweka kumbukumbu zao.
Kitu cha ziada kabisa kutokea uwanjani hapo ni baadhi ya vijana wa jeshi waliokuwa karibu na jukwaa hilo kukodolea macho mara kwa mara kwenye jukwaa hilo la akina Wema na Idrisa huku baadhi ya wanajeshi hao walisikika wakinong’onezana na kuonyesha mahala alipokuwa amekaa Wema.
Hakika hii ilikuwa ni kitu cha kipekee kwani wengi wa wananchi wakiwemo vijana wa kike walivutika kufika kwenye jukwaa hilo ikiwemo hata kukaa kwa mbali ilimradi tu wamshuhudia Wema na hali hiyo ilijidhihirisha kwani hata walipoondoka baadhi yao nao waliondoka katika jukwaa hilo.
Hii inaonyesha picha halisi kwani awali wasanii mbalimbali walifika kwenye jukwaa hilo lakini hawakupata shangwe zozote wala watu kuwafuatilia ila ujio huo pekee wa wawili hao uliibua shangwe za kushangilia na kufuatiliwa mara kwa mara na hata kupiga picha na ‘fans’ wao.
JPM1 (1)
Tukio la kihistoria la Dk. Magufuli kuapishwa lilivyokuwa katika jukwaa maalum leo Novemba 5, katika uwanja wa zamani wa Taifa maarufu Shamba la Bibi.