Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco Eng Cyprian Luhemeja akiongea na wafanyakazi kwenye mkutano na wafanyakazi
Ule
usemi maaarufu wa Hapa kazi tu” unaendelea kuimbwa na kufanyiwa kazi na
watanzazia wengi hususani watumishi wa Umma na serikali ili kuendana na kasi ya
awamu ya Tano ya Raisi Magufuli.
Kauli mbiu hiyo imekumbushwa tena na Afisa
Mtendaji Mkuu wa Dawasco Eng Cyprian Luhemeja wakati wa kikao cha pamoja na wafanyakazi wa shirika hilo mapema wiki hii.
“lazima
tuendane na kasi na speed ya Mheshimiwa Rais, tabia ya kufanya kazi kwa mazoea,
kutojali malalamiko ya Wateja sasa ni mwisho” aliongeza Luhemeja
Aliwataka
wafanyakazi kujali muda wao wa Kazi kwa kutenda yale ambayo yataondoa kero ya
Maji kwa Wateja hususani kuziba mivujo ya Maji katika maeneo mengi ya Jiji
pamoja na kupambana na wizi wa Maji ili kila mwananchi apate huduma ya Maji
kihalali.
Alimalizia
kwa kuwataka wafanyakazi wa DAWASCO kutekeleza kauli ya Rais aliyoitoa mapema
wakati akifungua Bunge katika sekta ya Maji pale aliposema “LAZIMA TUWATUE KINA MAMA NDOO KICHWANI”
kwa kuhakikisha huduma ya Maji inamfikia mwananchi na kuondokana na malalamiko
ya upatikanaji huduma hiyo kwa maeneo stahili.

wafanyakazi wa Dawasco wakimsikiliza Afisa mtendaji Mkuu kwenye mkutano na wafanyakazi wote makao makuu ya shirika hilo Gerezani


0 comments:
Post a Comment