Mrembo huyo akijigaragaza kwenye matope.
Tukio hilo la aina yake lilijiri hivi karibuni maeneo ya Mtaa wa CCM mjini hapa ambapo wanachama wa chama hicho walikodi muziki na kushangilia ushindi huo.
Baadhi ya wanachama wa chama hicho walipozungumza na gazeti hili walisema mkazi huyo ni shabiki mkubwa wa chama hicho na alikuwa akiwatania wanachama wa vyama vya upinzani kuwa, wataweza kukitoa chama hicho kwenye udiwani na ubunge, lakini siyo urais. Hivyo, ushindi wa Magufuli ulisababisha mkazi huyo kuwa na furaha ya kupitiliza huku akiwa amegida ulabu kwa ajili ya kushangilia. Mbaya zaidi huku mvua ikinyesha kwa mbali, alijitupa ndani ya tope na kuendelea kucheza muziki.
0 comments:
Post a Comment