Tuesday, November 3, 2015

PhotoGrid_1446451221225
 Jumanne iliyopita maeneo ya Buguruni Sukita kulitokea tukio la kinyama ambapo vijana wawili wakiume mmoja akikisiwa kuwa na umri wa miaka 14 waliuwawa kinyama kwa kuchomwa moto huku mwanamke mmoja akinusurika kufa baada ya kufanyiwa vitendo vya kinyama na kupelekea kuchomwa moto.
Tukio hilo lilitokea majira ya asubuhi ambapo kwa mujibu wa wakazi waeneo hilo wanasema watu wengi walikuwa bado wamelala ila walishitushwa na milio ya pikipiki ambazo zilikuwa zikisikika zikieleka huko maeneo ya sukita. Mpaka wanashituka kwenda kuwafwatilia walikuta tayari vijana wawili wameshachomwa moto kwakile wanachodai ni wezi wa Pikipiki.
Baada ya hapo waliweza kuondoka na kuja na huyo msichana akiwa hana nguo wakaanza kumpiga na kumfanyia vitendo vya kinyama na mwishowe kuanza kumchoma moto lakini wakazi waeneo hilo walikuwa tayari wengi washafika nakuwasihi wasifanye hivyo lakini walishindwa kuwazui kwakua hao vijana wa bodaboda walikuwa wengi.Lakini baada ya muda askari waliweza kufika katika eneo hill nakiweza kumuokoa dadahuyo. Ambapo kwa sasa yupo hospitali hali yake ikiwa mbali.
Niliweza kuongea na wakazi wa eneo ambao walishuhudia tukio hilo la kinyama
Moja ya wakazi wa eneo hilo akielezea tukio hilo la la kinyama lilivyokuwa
Jumanne iliyopita maeneo ya Buguruni Sukita kulitokea tukio la kinyama ambapo vijana wawili wakiume mmoja akikisiwa kuwa na umri wa miaka 14 waliuwawa kinyama kwa kuchomwa moto huku mwanamke mmoja akinusurika kufa baada ya kufanyiwa vitendo vya kinyama na kupelekea kuchomwa moto.
Tukio hilo lilitokea majira ya asubuhi ambapo kwa mujibu wa wakazi waeneo hilo wanasema watu wengi walikuwa bado wamelala ila walishitushwa na milio ya pikipiki ambazo zilikuwa zikisikika zikieleka huko maeneo ya sukita. Mpaka wanashituka kwenda kuwafwatilia walikuta tayari vijana wawili wameshachomwa moto kwakile wanachodai ni wezi wa Pikipiki.
Baada ya hapo waliweza kuondoka na kuja na huyo msichana akiwa hana nguo wakaanza kumpiga na kumfanyia vitendo vya kinyama na mwishowe kuanza kumchoma moto lakini wakazi waeneo hilo walikuwa tayari wengi washafika nakuwasihi wasifanye hivyo lakini walishindwa kuwazui kwakua hao vijana wa bodaboda walikuwa wengi.Lakini baada ya muda askari waliweza kufika katika eneo hill nakiweza kumuokoa dadahuyo. Ambapo kwa sasa yupo hospitali hali yake ikiwa mbali.
Niliweza kuongea na wakazi wa eneo ambao walishuhudia tukio hilo la kinyama
Moja ya wakazi wa eneo hilo akielezea tukio hilo la la kinyama lilivyokuwa

 

0 comments:

Post a Comment