"Tumefunga geti la ofisi za Wizara ilipofika saa 1:30 asubuhi. Tunataka watumishi wa Wizara wawahudumie wateja wetu Kwa tija na ufanisi.
Mimi nitawajibika kazini. Kila mtu atapaswa kuwajibika. Haya ndiyo mahitaji ya wakati huu. Leo nimefungia wachelewaji kazini nje ya geti. Nitaendelea kushughulika na watoro na watorokaji. Nasubiri ripoti ya watendaji kuhusu trend ya watumishi wote watoro, wachelewaji kisha nichukue hatua stahiki! Ili kazi ziende ni lazima tuweke nidhamu ya kazi Na uwajibikaji maofisini."
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla akiwaamrisha
askari wa getini wizarani hapo kuweka kufuli na kutoruhusu mtumishi yoyote wa ofisi hiyo kuingia ndani ya ofisi
za wizara ilipotimu saa 1:32 asubuhi mapema leo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla akisimamia
zoezi la ufungwaji wa geti hilo, Kulia ni askari wa SUMA JKT akiweka kufuli katika lango kuu la kuingia katika
ofisi za Wizara ya Afya.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla akiwauliza
askari wa getini kuhusu daftari la mahudhurio ya watumishi wa wizara baada ya kufungwa geti hilo,
na kupewa maelezo kuwa watumishi huonyesha vitambulisho pekee na husaini katika vitengo vyao.
Mmoja wa wafanyakazi wa Wizara ya Afya akiwasili ofisini huku muda wa kuingia kazini ukiwa umepitiliza.
Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla
akizungumza na mmoja watumishi wa wizara hiyo na kuagiza kuletewa vitabu vya mahudhurio kwa vitengo vyote
vilivyopo wizarani hapo.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Afya, Michael John akitoa maelezo kuhusu
mahudhurio ya watumishi kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla.
Magari ya watumishi wa Wizara ya Afya yakiendelea kuwasili ofisini bila ya kutambua kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri,
Dkt. Kigwangalla ametoa agizo la kuizuia watumishi wachelewaji.
Askari wa getini wakimpa maelezo mmoja wa watumishi wa wizara hiyo kuwa Mh. Naibu Waziri ameagiza
watumishi wote waliochelewa kuzuiliwa kuingia ndani.
Mmoja wa wasaidi wa idara ya rasilimali watu akimkabidhi vitabu vya mahudhurio Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla akipitia
mahudhurio ya watumishi wa wizara kwa siku zilizopita.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla akipitisha
mstari wa kufunga mahudhurio kwa watumishi ambao wameripiti kabla ya saa 1:30 asubuhi ya leo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla
akiendelea na zoezi hilo la kupitisha mstari kwa kila idara za wizara hiyo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla akizungumza
na waandishi wa habari kuhusu juu ukaguzi huo katika ofisi za wizara yake ya afya ili kuboresha
utendaji wa wizara hiyo na vituo vyote vya sekta ya afya nchini kote.
Aidha Naibu Waziri huyo alimtaka Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kuhakikisha watumishi wote waliochelewa kufika ofisini wanaandika barua ya kutoa maelezo kwanini wanachelewa kufika ofisini na baada ya hapo Mkurugenzi na yeye atoe maelezo kwanini muda wa kutoka watumishi wanakuwa hawasaini kuwa wametoka.
Mh. Kigwa akitoa maelekezo kwa SUMA JKT kfunga geti kwa kufuli kubwa la Solex , kisha wamkabidhi funguo za geti yeye, yeye alifika saa moja kamili asubuhi , tena alikuja kwa miguu. ilipofika saa 1:32 akatoka nje ya geti na kuanza mtachokiona hapo chini. Twende kazi.
Kigogo mzito wa wizara ya Afya akiwa kafungiwa geti baada ya kuchelewa kufika kazini.
Hapa kigogo akiomba kupata upenyo wa kupitishwa japo mlango wa uani (mlango wa chobingo),
lakini walinzi waka mkazia kavu kavu. mara ghafla kijasho chembamba kikaanza kumtoka kwapani
ingawa ilikuwa ni asubuhi na upepo ukivuma kwa kasi.
akikabidhiwa daftari la mahudhurio ya wafanyakazi kutoka kwa afisa Rasilmali watu
akaanza kukagua mahudhurio yanavyojazwa , akakuta vituko viwili vikubwa, kwanza
1.majina ya wafanyakzi yameisha andikwa kuwa wako kazini ndani ya muda (kabla ya saa moja na nusu)
2. watu wanapigiana sahihi kisela hata kama haujafika au hutokuja kazini kabisa.
NB: kuepusha hiyo manual ssytem ya kusainiana, ameagiza waanze utaratibu wa ku punch kwa
kutumia electronic system ambapo mtu anaweka finger print wakati wa kuingia kazini na kutoka ofisini.
ofisi nyingi sana hasa za wahindi huu ndio mfumo unaotumika.
Akapitisha mstari MKUUBWAAA tena MWEKUNDUUUU....ili wataokuja wasaini chini yake.
Mh. kigwagz anajifanya kamzkazia kavu mnyamwezi ,
na jamaa anatabasamu tu .
0 comments:
Post a Comment