Tuesday, December 1, 2015

Roch Marc Christian Kabore

Roch Marc Christian Kabore ameshinda uchaguzi mkuu wa nchi hiyo, kwa mujibu wa tume ya uchaguzi.

Waziri Mkuu huyo wa zamani alipata alisimia 53 nukta tano hivyo amepata ushindi wa moja kwa moja, kwa kuzoa zaidi ya asili mia 50.
Huu ndio uchaguzi mkuu wa kwanza tangu maandamano yaliyomuondoa madarakani Rais wa miaka mingi Blaise Compaore.
Uchaguzi Mkuu ulitarajiwa kufanyika mwezi uliopita lakini ukacheleweshwa na jaribio la mapinduzi ambalo halikufaulu hapo mwezi Septemba.
Bwana Compaore anaishi uhamishoni katika nchi jirani ya Ivory Coast.

0 comments:

Post a Comment