Msanii Nassib Abdul maarufu kama”Diamond Platinumz” anatarajiwa
kuungana na wasanii wenzake akiwemo Msaga Sumu, kikundi cha wakali
Dancer kwa ajili ya kutumbuiza kwenye tamasha maalum litakalofanyika
desemba 25 mwaka huu jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa mratibu wa onesho hilo Juma Mbizo, amesema Tamasha
linalenga kuhakikisha mashabiki na wapenzi wa burudani nchini wanamaliza
mwaka 2015 na kuingia 2016 kwa kupata burudani ya aina yake kutoka kwa
mkali huyo wa kimataifa pamoja wasanii wengine wa nyumbani.
Kwa upande wake Diamond Mwenyewe amesema ataendelea kufanya kama
kawaida yake kwa kuhakikisha anatoa kile mashabiki wanachokihitaji
katika burudani pindi anapokuwa stejini.

0 comments:
Post a Comment