Saturday, December 12, 2015




Msanii anayefanya poa na ngoma yake ya TOBA, malikia wa uswazi maarufu kama Shaa, amefunguka na kusema vitendo vilivyo kuwa vinafanyika katika video yake havihusiani na Freemason

 Shaa amesema amekuwa akiulizwa na watu mbalimbali kuhusu hilo swala na amekutana na maoni mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii lakini amezidi kusisitiza kuwa hausiki na masuala hayo kwani kuwa Freemasson lazima uwe na pesa za kutosha.

 Pia shaa ameelezea kuwa yupo mbioni kufanya kolabo na mfalme wa uswazi Msaga Sumu kwani anaamini msanii huyo anafanya vizuri, hivyo wakikutana na kufanya kazi pamoja itakuwa vizuri zaidi.

0 comments:

Post a Comment