KAMPUNI
ya serikali inayotoa huduma za meli katika eneo la Maziwa Makuu, Marine
Services Company Ltd (MSCL), inadaiwa kutumia kinyume sh.milioni 300
kati ya milioni 600 ilizokuwa imepewa kutengeneza meli ya Mv.Victoria.
Hali
hiyo iligunduliwa na Mkuu wa Mkoa (RC) wa Mwanza Magesa Mulongo baada
ya kutembelea ofisi za kampuni hiyo zilizopo Bandari ya Mwanza
Kaskazini.
Uongozi
wa MSCL unadaiwa kutumia fedha hizo kulipa mishahara badala ya
kutengeneza meli hiyo iliyojengwa mwaka 1964, ambayo kwa zaidi ya mwaka
mmoja sasa imeegeshwa katika Bandari ya Mwanza Kusini, kutokana na
kuharibika kwa baadhi ya mitambo na kangavuke (Generator) ya kufua
nishati ya umeme melini.
Hali hiyo imewaathiri vibaya abiria na wasafirishaji wa mizigo kati ya Mwanza na Bukoba.
Desemba
mwaka jana Mv Victoria ilipandishwa kwenye chelezo ili ifanyiwe
matengenezo,kazi iliyopaswa kuanza Julai mwaka huu, lakini haikufanyika
kutokana na fedha kukosekana; hivyo ikashushwa kutoka kwenye chelezo.
Imedaiwa
kuwa matengenezo ya meli hiyo inayotegemewa na wakazi wa Mikoa ya
Mwanza na Kagera,yamekwama kutokana na kiasi cha fedha kutumika kulipa
mishahara ya wafanyakazi na kiasi kingine kununua vipuri kwa ajili ya
kufanyia ukarabati wa meli nyingine (Mv.Serengeti) kinyume na maelekezo
ya serikali.
0 comments:
Post a Comment