Monday, December 21, 2015



 

Zaidi ya magogo ya asili 5000 pamoja na makontena 20 yaliyojaa magogo yamekamatwa na wakala wa misitu nchini katika mpaka wa Tanzania na Zambia mjini Tunduma, yakisafirishwa kinyume cha sheria huku yakiwa hayajulikani yanakotokea.
Magogo hayo yamekamatwa yakiwa kwenye mpaka wa Tanzania na Zambia mjini Tunduma kufuatia doria ambayo imefanywa na maofisa wa wakala wa misitu nchini.
 
Mkurugenzi huyo wa wakala wa misitu nchini, Mohamed Kilongo amesema mbali na magogo hayo pia wamezuia usafirishaji wa makontena 20 ambayo yameingizwa nchini kutokea Zambia yakiwa yamebeba magogo, hatua inayotokana na usafirishaji huo kukiuka makubaliano baina ya nchi hizo mbili ya kutoruhusu usafirishaji wa magogo ya aina hiyo.
 
Hata hivyo meneja wa idara ya maliasili  wa Zambia, Adotey Addo amesema nchi yake imetoa kibali cha kuruhusu usafirishaji wa makontena 20 ya magogo, na kwamba mbali na makontena hayo, magogo mengine ambayo yamekatwa ni haramu.
 
Baadhi ya mawakala wa kampuni za usafirishaji, Clearing and Forwarding ambao wameshughulikia usafirishaji wa magogo hayo wamesema sio jukumu lao kujua kama mzigo wanausafirisha ni halali au haramu kwa kuwa hilo ni jukumu la idara ya forodha.
 

0 comments:

Post a Comment