Thursday, December 24, 2015



Mtangazaji na msanii wa kundi la muziki wa dansi la Mapacha Watatu ameeleza kuwa katika maisha yake ya kimuziki aliwahi kutunzwa kiasi cha dola 1000 za kimarekani na kuongeza kuwa katika utunzwaji wa wasanii kunachangamoto mbalimbali ambazo usipokuwa makini unaweza kujikuta unamsaliti mkeo au mpenzi wako.


 Akizungumzia changamoto hizo Jose Mara amesema kuwa unaweza ukatunzwa kiasi Fulani cha pesa na kukuta pesa hizo zimeandikwa namba za simu za aliyekutunza  na kueleza kuwa upande wake Jose Mara amesema yeye hawezi kushawishika kumsaliti mke wake kwani anamuheshimu na haitaji kuugua maradhi yanayosababishwa na ngono nzembe.

 Vilevile Jose Mara amevitaka vyombo vya habari kuunga mkono mziki wa dansi kama wanavyofanya kwenye aina nyingine ya muziki kwani kutouunga mkono ni kuua mziki huo

0 comments:

Post a Comment