Sunday, December 6, 2015

 


MGOMBEA Urais nchini Marekani kwa tiketi ya chama cha Democratic,Bi Hillary Clinton ametamba kuwa endapo atachaguliwa kuliongoza taifa hilo katika uchaguzi mkuu ujao moja ya kipaumbele chake cha kwanza ni kuhakikisha suala la afya ya uhakika linakuwa kipaumbele kwa kila Mmarekani.

Bi Hillary ambaye atambana na mgombea wa chama cha Republican Donald J Trump amesema kuwa atahakikisha kila Mmarekani anayestahili kupata huduma bora za afya anapata bila kujali hali yake ya uchumi 

Uchaguzi Mkuu wa marekani unataraji kufanyika mwakani huku joto kubwa la uchaguzi huo likiwa katika wagombea wa vyama viwili vya Democratic na Republican ambayo vimekuwa vikibadilishana madaraka kila mara baada ya miaka minne au nane ya utawala wa Rais aliyeko madarakani


0 comments:

Post a Comment