Friday, December 18, 2015



 
 
Majira ya saa 10 na dakika 10 Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Mhongo alifika katika mitambo ya kuzalisha umeme wa gesi iliyoko  Tegeta jijini Dar es Salaam inachomilikiwa na Tanesco bila ya kutoa taarifa na kukuta wafanyakazi pamoja na wahandisi wa kituo hicho cha umeme wakiendelea na kazi katika mitambo hiyo. 

 
Waziri Muhongo amekagua  mitambo hiyo leo  na kubaini kuwa umeme uniti moja inatengenezwa kwa gharama ya shilingi 90 na kuuzwa kwa wananchi kwa shilingi 180 ikiwa ni kiwango kikubwa kwa mwananchi wa kawaida.
 
Pia Muhongo amesisitiza kuwa umeme unatakiwa kushuka bei ili kila mwananchi anufaike na nishati hiyo  hapa nchini.

0 comments:

Post a Comment