Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa amesema wanasiasa walioshindwa kwenye Uchaguzi
Mkuu hawaruhusiwi kuitisha mikutano ya hadhara kwa ajili ya kuwashukuru
wananchi kwa kuwa wanaweza kuvuruga shughuli za maendeleo.
Waziri
Mkuu alisema hayo wakati akilishukuru Jeshi la Polisi wilayani Ruangwa
kwa kufanya kazi ya kusimamia Uchaguzi Mkuu uliomalizika Oktoba 25 kwa
CCM kushinda kiti cha urais na kuzoa takriban viti 180 vya ubunge.
“Naendelea
kuwashukuru kwa mchango wenu mkubwa kiulinzi, lakini pia usimamizi wa
zoezi zima la uchaguzi na hatimaye hivi sasa watu wameshapatikana,” alisema Waziri Majaliwa nje ya ofisi za jeshi hilo.
“Na
tumesema, siasa tumeshazimaliza. Sasa tunataka tufanye kazi za
maendeleo. Hatuhitaji tena watu kuja kutuvuruga. Mikutano ya shukrani
itafanywa na wale tu walioshinda kwenye maeneo yao. Wengine watulie.
“Vyama
sasa viache wale tu waliochaguliwa kwenye maeneo yao washukuru, wengine
hawa watakuja kuleta maneno ambayo yatatuvuruga. Mimi naamini mko
imara.”
Wakati
Waziri Majaliwa akisema hayo, tayari Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea
urais wa Chadema na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi
(Ukawa), alishapanga kuanza ziara ya kuzunguka nchi nzima kwa lengo la
kuwashukuru wananchi waliompigia kura.
Hata
hivyo, ilipofika siku ya kuanza ziara hiyo, Chadema ilitangaza kuwa
imeahirisha hadi itakapotangazwa tena, ikiweka bayana kuwa uamuzi huo
hautokani na vitisho vya makamanda wa polisi wa mikoa

0 comments:
Post a Comment