Tuesday, December 29, 2015

 
 
BAADA ya kushughulikia wakwepa kodi ndani ya siku 27 alizokaa Mamlaka ya Mapato (TRA), Waziri mpya wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amehamishia nguvu zake katika sekta ya fedha hasa benki, akizitaka zipunguze riba.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Ikulu Dar es Salaam jana, baada ya kuapishwa na Rais John Magufuli, Dk Mpango aliahidi kushughulikia tatizo la riba kubwa, inayotolewa kwenye benki za hapa nchini, jambo linalochangia kushusha idadi ya watu wanaokwenda benki kukopa.
 
“Lazima sekta ya fedha isimamiwe vizuri ili kila mwananchi aweze kukopa, nitahakikisha riba za mikopo zinashuka ili wananchi wajipatie mikopo kwa riba nafuu,” alisema Dk Mpango.

0 comments:

Post a Comment