Tuesday, December 15, 2015


 
 
Wakazi wa jimbo la kibamba wamemtaka mbunge wao, John Mnyika kuanza kufanyia kazi ahadi zake badala ya kuanza kutoa matamko kwenye vyombo vya habari kuzungumzia mambo ya kitaifa wakati ana mambo kadhaa ya kuyafanyia kazi jimboni kwake.

Mkazi kibamba aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Uledi maarufu kama ‘Mzee wa Ukawa’ alisema “Mnyika si mgeni na matatizo ya Kibamba kwani hili lilikuwa ni eneo lake alipokuwa mbunge wa Ubungo. Hivyo hatutegemei kumwona akitumia muda mrefu kuongelea mambo ya kitaifa badala ya kushughulikia kero zetu.”

“Tunamtaka Mbunge wetu arudi jimboni kukaa na sisi ili atueleze mikakati aliyonayo na pia muda wa kuanza kutimiza ahadi alizotuahidi badala ya kuanza kulalamikia suala la ofisi aliyopewa kuwa ndogo. Hivi sasa kipaumbele chake kiwe kero zetu badala ya kufikiria kuanza kukaa ofisini,” alisema Mwanaisha Swedi akiwa katika sehemu yake anayofanyia biashara ya kuuza vitafunio.

"Tunamtaka mbunge wetu aache kulalamikia suala la ofisi, aje atuambie nasi tuna uwezo wa kumjengea ofisi kubwa katika eneo hili. Tunamtaka aje aungane nasi kujikwamua kwenye matatizo yetu ya kiuchumi na kimiundo mbinu" alisema Jerome Munishi ambaye alijitambulisha kuwa ni mkazi wa mbezi mwisho.
 
STORY NA DAR24

0 comments:

Post a Comment