Wakazi
wa jimbo la kibamba wamemtaka mbunge wao, John Mnyika kuanza kufanyia
kazi ahadi zake badala ya kuanza kutoa matamko kwenye vyombo vya habari
kuzungumzia mambo ya kitaifa wakati ana mambo kadhaa ya kuyafanyia kazi
jimboni kwake.
Mkazi kibamba aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Uledi maarufu kama ‘Mzee wa Ukawa’ alisema
“Mnyika si mgeni na matatizo ya Kibamba kwani hili lilikuwa ni eneo
lake alipokuwa mbunge wa Ubungo. Hivyo hatutegemei kumwona akitumia muda
mrefu kuongelea mambo ya kitaifa badala ya kushughulikia kero zetu.”
“Tunamtaka
Mbunge wetu arudi jimboni kukaa na sisi ili atueleze mikakati aliyonayo
na pia muda wa kuanza kutimiza ahadi alizotuahidi badala ya kuanza
kulalamikia suala la ofisi aliyopewa kuwa ndogo. Hivi sasa kipaumbele
chake kiwe kero zetu badala ya kufikiria kuanza kukaa ofisini,” alisema Mwanaisha Swedi akiwa katika sehemu yake anayofanyia biashara ya kuuza vitafunio.
"Tunamtaka
mbunge wetu aache kulalamikia suala la ofisi, aje atuambie nasi tuna
uwezo wa kumjengea ofisi kubwa katika eneo hili. Tunamtaka aje aungane
nasi kujikwamua kwenye matatizo yetu ya kiuchumi na kimiundo mbinu" alisema Jerome Munishi ambaye alijitambulisha kuwa ni mkazi wa mbezi mwisho.
STORY NA DAR24

0 comments:
Post a Comment