Saturday, January 2, 2016

 


TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilayani Igunga mkoani Tabora,  imemfikisha mahakamani daktari Salumu Rashidi (58) aliyegoma kumtibu mtoto wa miaka miaka miwili.

Mwendesha mashitaka wa taasisi hiyo, Aidan Samali alimsomea Rashidi shitaka lake mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Igunga, Ajali Milanzi.

Samali alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Desemba 21, mwaka huu, katika Hospitali ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora.

Alidai kuwa Rashidi ni mtumishi wa hospitali  hiyo anadaiwa kuomba rushwa ya sh. 40,000 kutoka kwa Gigwa Malale mkazi wa Kijiji cha Mgongoro ili aweze kumpatia matibabu mwanawe Nkamba Mbusule aliyekuwa ameingiwa na punje ya mahindi puani.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa ya mwaka 2007, kinachozuia kutenda makosa kama hayo.

Hata hivyo, Rashidi alikana shitaka lake na kurudishwa mahabusu baada ya kukosa mdhamini. Kesi hiyo itatajwa tena Januaria 11, mwaka huu.

0 comments:

Post a Comment