RAIS
Dk. John Magufuli, amesema Watanzania wote wanapaswa kuendelea
kumuombea ili aendelee na kazi yake ya kupambana na mafisadi wahujumu
uchumi na vigogo wauza dawa za kulevya nchini.
Kauli
hiyo iliitoa katika mkesha mkubwa wa kuliombea Taifa pamoja na kuuaga
mwaka 2015 na kuukaribisha mwaka 2016, uliofanyika kwenye Uwanja wa
Uhuru jijini Dar es Salaam.
Rais
Magufuli amesema Taifa hili kwa kipindi kirefu lilikabiliwa na vigogo
wauza dawa za kulevya, watumishi na vigogo wakwepaji wa kodi pamoja na
wizi wa dawa mahospitalini hivyo viongozi wa dini na Watanzania wote
wanapaswa kumuombea ili aweze kutumbua majipu ya mafisadi hao.
Amesema
ubadhilifu wa mali za umma umekuwa ukichangia kuzorotesha maendeleo ya
Watanzania wote kutokana na watu wachache wasiokuwa waadilifu serikalini
kuendelea na vitendo vya rushwa huku wengi wakiendelea kutaabika.
Dk.
Magufuli ambaye aliwakilishwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo na
Makazi, William Lukuvi, amesema kuwa viongozi wa dini wanapaswa
kuendelea kuliombea Taifa na kuwaombea watu wabaya wasiopenda maendeleo
waweze kubadilika ili nchi iweze kusonga mbele.
“Viongozi
wa dini tunapaswa kuendelea kumuombea rais wetu (Dk. John Magufuli)
aendelee kutumbua majipu haya ambayo yanasababisha maendeleo ya Taifa
letu kurudi nyuma.

0 comments:
Post a Comment