Saturday, January 2, 2016


 
 
RAIS Dk. John Magufuli, amesema Watanzania wote wanapaswa kuendelea kumuombea ili aendelee na kazi yake ya kupambana na mafisadi wahujumu uchumi na vigogo wauza dawa za kulevya nchini.

Kauli hiyo iliitoa katika mkesha mkubwa wa kuliombea Taifa pamoja na kuuaga mwaka 2015 na kuukaribisha mwaka 2016, uliofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli amesema Taifa hili kwa kipindi kirefu lilikabiliwa na vigogo wauza dawa za kulevya, watumishi na vigogo wakwepaji wa kodi pamoja na wizi wa dawa mahospitalini hivyo viongozi wa dini na Watanzania wote wanapaswa kumuombea ili aweze kutumbua majipu ya mafisadi hao.

Amesema ubadhilifu wa mali za umma umekuwa ukichangia kuzorotesha maendeleo ya Watanzania wote kutokana na watu wachache wasiokuwa waadilifu serikalini kuendelea na vitendo vya rushwa huku wengi wakiendelea kutaabika.

Dk. Magufuli ambaye aliwakilishwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo na Makazi, William Lukuvi, amesema kuwa viongozi wa dini wanapaswa kuendelea kuliombea Taifa na kuwaombea watu wabaya wasiopenda maendeleo waweze kubadilika ili nchi iweze kusonga mbele.

“Viongozi wa dini tunapaswa kuendelea kumuombea rais wetu (Dk. John Magufuli) aendelee kutumbua majipu haya ambayo yanasababisha maendeleo ya Taifa letu kurudi nyuma.

0 comments:

Post a Comment