Saturday, January 9, 2016

Dr. Kiiza Besigye.
 
 
MGOMBEA  urais nchini Uganda kwa tiketi ya chama cha Forum for democratic change-FDC Dr. Kiiza Besigye, ametoa changamoto kwa mwenzake wa chama tawala cha National resistance movement-NRM rais Yoweri Museveni, kutokwepa mdahalo wa pamoja wa wagombea wote wa urais unaotarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa wiki ijayo...,
 
Hii ni baada ya rais Museveni kusema kwamba hana muda wa kutosha kuhudhuria mjadala huo kutokana na ratiba  zake za kampeni akisema anahutubia  mikutano minne ya kampeni kila siku.
 
 Besigye alikuwa akihutubia umati mkubwa wa watu mashariki mwa Uganda katika mji wa Mbale akiwa kwenye uwanja mmoja mjini humo uliojaa watu kupita kiasi.
 
Mdahalo huo umeandaliwa na taasisi za kidini na  Besigye anasema itawapa wananchi wa Uganda kuchambua mbivu na mbichi kisiasa.

0 comments:

Post a Comment