Mariah Carey na James Packer.
DIVA wa muziki duniani, Mariah Carey amepanga kuolewa na bilionea maarufu wa Australian, James Packer.
Hii imedhihirika juzi usiku baada ya Packer, mwenye umri wa miaka 47, kumvisha pete ya almasi (yenye thamani ya dola za Marekani milioni 7.5)
mwanamama Carey, mwenye umri wa miaka 45, tukio likifanyika mbele ya umati wa marafiki wa karibu wa Carey wakati wa chakula cha usiku kwenye mgahawa wa Eleven Madison Park huko New York.
Wapenzi hao wamekuwa katika mahusiano kwa takribani mwaka mzima sasa tangu waliopokutana kwa mara ya kwanza mwaka 2014 kupitia rafiki wa Packer Brett Ratner hyuko Aspen, walianza kuwa marafiki wa kawaida na baadaye wakawa wapenzi.

0 comments:
Post a Comment