Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekutana
na kufanya mazungumzo na viongozi wanne Ikulu Jijini Dar es salaam
ambapo pamoja na kutakiana heri ya Mwaka Mpya, wamezungumzia mambo
mbalimbali kuhusu mustakabali wa Serikali ya awamu ya Tano ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
Akizungumzia
yaliyojiri katika Mazungumzo hayo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali (CAG) Profesa Mussa Juma Assad amesema wamezungumzia kupunguza gharama za matumizi ya kuendesha serikali na kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali.
Profesa
Assad amebainisha kuwa Rais Magufuli ametaka Ofisi ya Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ihakikishe Tanzania inaongeza
ukusanyaji wa mapato kutoka asilimia 14 ya pato la Taifa (GDP) kwa
mujibu wa hesabu zilizofanyika mwaka juzi.
"Hadi
Mwaka juzi Tanzania ilikua inakusanya mapato kwa kiwango cha asilimia
14 ya pato la Taifa ikilinganishwa na Kenya ambayo ilikua ikikusanya
asilimia 19 ya pato Taifa, na hakuna sababu za Msingi za kwa nini
Tanzania iwe nyuma katika ukusanyaji wa mapato hayo" aliongeza Profesa Assad.

0 comments:
Post a Comment