Rais
John Magufuli amemaliza mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa Kapunga
na mwekezaji wa Kapunga Rice Project Limited na sasa hekta 1,780
zitakuwa mali ya wananchi.
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alitangaza jana
katika mkutano wa hadhara ambao licha ya mvua kubwa, wananchi
walimsikiliza kwa makini na kushangilia baada ya kupokea taarifa hiyo.
Kijiji cha Kapunga kina wananchi 4,500.
Lukuvi alisema hatua hiyo ni zawadi ya kwanza ya Rais kwa wananchi Tanzania kwa kutatua mgogoro wa siku nyingi.
“Rais
amedhamiria kuwasaidia wananchi, hivyo naomba (Mkuu wa Mkoa), uandae
orodha ya watu wote wanaomiliki mashamba yasiyoendelezwa ingawa wanapata
mikopo kupitia hati za mashamba hayo ili kazi ya Serikali kuwapatia
maeneo ya kulima na wananchi wa kawaida iweze kufanikiwa,” alisema.
Lukuvi
alikwenda kwenye kijiji hicho kutangaza jambo ambalo aliyekuwa waziri
wa wizara hiyo, Profesa Anna Tibaijuka alilishindwa Januari 7, 2013.
Meneja
wa Mradi Kapunga Rice Project, Sumil Tayic alisema viongozi wake
wameafiki uamuzi wa Rais bila kinyongo na sasa wataimarisha ushirikiano
mzuri na wananchi.

0 comments:
Post a Comment