Tuesday, January 5, 2016

 


Rais John Magufuli amemaliza mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa Kapunga na mwekezaji wa Kapunga Rice Project Limited na sasa hekta 1,780 zitakuwa mali ya wananchi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alitangaza jana katika mkutano wa hadhara ambao licha ya mvua kubwa, wananchi walimsikiliza kwa makini na kushangilia baada ya kupokea taarifa hiyo. Kijiji cha Kapunga kina wananchi 4,500.
Lukuvi alisema hatua hiyo ni zawadi ya kwanza ya Rais kwa wananchi Tanzania kwa kutatua mgogoro wa siku nyingi.
“Rais amedhamiria kuwasaidia wananchi, hivyo naomba (Mkuu wa Mkoa), uandae orodha ya watu wote wanaomiliki mashamba yasiyoendelezwa ingawa wanapata mikopo kupitia hati za mashamba hayo ili kazi ya Serikali kuwapatia maeneo ya kulima na wananchi wa kawaida iweze kufanikiwa,” alisema.
Lukuvi alikwenda kwenye kijiji hicho kutangaza jambo ambalo aliyekuwa waziri wa wizara hiyo, Profesa Anna Tibaijuka alilishindwa Januari 7, 2013.
Meneja wa Mradi Kapunga Rice Project, Sumil Tayic alisema viongozi wake wameafiki uamuzi wa Rais bila kinyongo na sasa wataimarisha ushirikiano mzuri na wananchi.

0 comments:

Post a Comment