Monday, January 4, 2016

 

Wakati watanzania wanasheherekea kuingia kwa mwaka mpya kamanda wa polisi mstaafu kanda maalum ya Dar es Salaam kamishina mstaafu Suleimani Kova amekabidhi rasmi wadhifa huo kwa naibu kamishina Simon Sirro katika hafla fupi iliyo fanyika katika viwanja vya chuo cha maafisa wa jeshi hilo Kilwa road jijini Dar es Salaam baada ya yeye kustaafu kwa mujibu wa sheria.

Katika hafla hiyo ambayo imeambatana na maonyesho ya vitu mbalimbali ambavyo vimekamatwa katika uongozi wake zikiwemo nyara za serikali, silaa nzito, magari, pikipiki mabomu, nyavu na kuwatunukia zawadi askari na raia ambao wamefanya kazi nzuri za kufichua uhalifu, ambapo ameishukuru jamii, familia yake pamoja na vyombo vya habari kwa ushirikiano mzuri walio mpatia katika utekelezaji wa majukumu yake ambayo ameyataja kuwa hayakuwa rahisi.
 
Kwa upande wake kamanda mpya wa jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam naibu kamishina Simon Sirro amewataka askari polisi wa kanda hiyo kuachana na vitendo vya rushwa na kusisitiza yeyote atakaye kiuka taratibu za jeshi hilo hatua kali za kisheria ikiwemo kufukuzwa kazi zitachukuliwa juu yake.
 
Katika hatua nyingine kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Ilala ambaye amehudhuria hafla hiyo amesema jeshi hilo kwa ujumla limejipanga katika kuhakikisha sherehe za mwaka mpya zinapita kwa amani na utulivu huku wafanya biashara wa china wakikabidhi pikipiki 3 kwa jeshi hilo kituo cha Msimbazi ambacho kipo chini ya kamanda huyo.

0 comments:

Post a Comment