Saturday, January 2, 2016

Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamefurika katika ufukwe wa koko na kumpongeza rais Dkt John Magufuli kwa uamuzi wake wa kutaka ufukwe huo uendelee kuwa wa wananchi wote hususani wenye uwezo wa hali ya chini ili waweze kufurahi ndani ya nchi yao.


ITV imetembelea katika ufukwe huo wa koko na kukuta zaidi ya watu elfu 10 wakiwa wamepumzika na wengine wakiogelea wakisherehekea mapumziko ya siku ya mwaka mpya ambapo wakizungumza na ITV wamesema rais Magufuli ameonekana kujali zaidi wanyonge wenye uwezo mdogo na kusisitiza kwa upande wao hawana uwezo kulipa fedha ili waweze kustarehe katika fukwe hizo. 
 
Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara ndogondogo wameitaka serikali kutoruhusu sehemu hiyo kuweka mifumo itakayotaka wananchi kulipa kiingili kwa kuwa kufanya hivyo kutapunguza idadi ya wananchi wanaotembelea ufukwe huo hali inayoweza kukwamisha biashara zao.

0 comments:

Post a Comment