Mwenyekiti
wa chama cha ACT- Wazalendo ,Anna Mughwira amewahimiza waandishi wa
habari mkoani hapa, kutumia taaluma yao kuwaelimisha wazazi/walezi juu
ya madhara watakayopata wanafunzi watoro, ili waweze kutoa ushirikiano
wa kukomesha vitendo hivyo.
Mwenyekiti
huyo ametoa wito huo wakati akishiriki ajenda ya utoro na mimba kwa
wanafunzi kwenye kikao cha kamati ya ushauri (RCC) mkoa kilichofanyika
katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa mjini hapa.
Alisema
vitendo vya utoro na mimba kwa wanafunzi havivumiliki, kwa madai
vinasababisha wahusika kukosa haki yao ya msingi ya kupata elimu.
“Kama
mnavyojua kuwa elimu ndio ufunguo wa maisha, elimu bora inamsaidia
mhusika kumudu maisha yake. Mwanafunzi awe mtoro wa reja reja au utoro
wa kudumu,anajikosesha haki yake ya msingi na kwa vyo vyote maisha yake
yatakuwa mabaya”,alisema.
Kwa hali hiyo,mwenyekiti huyo amewataka waandishi wa habari kuwa mstari wa mbele kukomesha vitendo vya utoro mashuleni.
“Waandishi
wa habari mliopo hapa, tumieni vizuri taaluma yenu kuwaelimisha na
kuwahamasisha wazazi kusimamia watoto wao kuhudhuria shuleni bila
kukosa,ili kuboresha taaluma na mwisho wa siku, wafanye vizuri kwenye
mitihani yao”, alifafanua Mughwira.

0 comments:
Post a Comment