Thursday, January 14, 2016



 

Aliyewahi kuwa mpenzi wa mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi maarufa kama Mr Sugu, Faiza Ally, ameamua kufanya kitu tofauti katika jamii baada ya kuandika kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa pesa zilizo patikana kwa njia ya kununua tiketi kwenye siku yake ya kuzaliwa atazielekeza kusaidia watoto yatima.

 


Jambo rafiki..... Kama nilivyo ahidi kuwa kila alie nunua tiketi kwenye birthday yangu kiasi hicho kitaenda kwa watoto yatima wkt huyo umekaribia kufanyika na nitatangaza lini niko kwenye mipango ambayo hivi karibuni itakamilika.... Pia wale wasomaji wazuri wa post zangu kama mna kumbukumbuku mara kazaa nilisha andika kuwa - wazazi wengi wenye uwezo kidogo mara nyingi watoto wao wanakua na vitu vingi wasivyo tumia au vimechakaa kwa wao- kama nguo-viatu- toys-vitabu vya shule hata vya dini vinakuaga vipo vipo humo majumbani hata magodoro - vyandarua mimi naomba tukusanye tupele huko vituoni maana watoto wa vituoni wana hitaji na vita wasaidia sana - ikiwa unaweza kutoa vipya ni sawa lkn hata vya zamani vitasaidia sana - kwa hivyo mwenye moyo wa kutoa aanze kujiandaa kabla ya mwisho wa mwezi nitatangaza siku maalumu ya kuleta hivyo vitu.... Unaweza ukaleta vyakula pia....na naomba wewe unae soma post hii mfahamishe na mwenzio kama una ndugu au rafiki ambae unajua watoto wake wana vingi wasivyo tumia muombe ili tukasaidie watoto wanao hitaji ... Pia naomba kama unajua kituo chochote cha yatima chenye hali mbaya zaidi nifahamishe kupitia number hii 0754242888 - maana kuna vituo vingine vinajulikana vina saidiwa na watu wengi hivyo ni vizuri tukajua vituo vingine zaidi ili tuwafikishie misaada yetu.....#watoto ni wetu ni jukumu letu #tushirikiane kwa uwezo tulio nao.......tag rafiki - naomba pia u share usapambaze ujumbe huu
A photo posted by Faiza Ally✨ (@faizaally_) on

0 comments:

Post a Comment