IKULU ya Kenya imemlipua mwanasiasa maarufu wa nchi hiyo Raila Odinga
kuwa amekuwa akiongoza kwa vitendo vya hujuma. Mbali ya hiyo, Ikulu
imesema Raila na washirika wake wakuu, Kalonzo Musyoka na Moses
Wetangula wanaandamwa na rekodi yao mbaya ya zamani kuhusiana na vitendo
vya rushwa na kuwa walikuwa wakitumia ofi si za serikali kwa manufaa
binafsi.
Habari zilisema, Ikulu juzi ilitupa makombora kwa Raila na kumhusisha
na vitendo vya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka ikiwa ni kipindi
kifupi baada ya kiongozi huyo kusema Serikali ya Muungano wa Jubilee,
imeshindwa.
Katika kutupiana makombora baina ya pande hizo, Ikulu inaonekana
kutayarisha video zilizorekodiwa maalumu kwa ajili ya kiongozi huyo wa
Mungano wa Cord ambaye alikuwa madarakani katika uongozi uliopita.
Uongozi wote wa Cord ulighubikwa na vitendo vya rushwa na wahusika
walitumia ofi si za umma kwa ajili ya kujinufaisha binafsi,ilisema
sehemu ya taarifa dhidi ya Raila. Iliongeza kuwa: ìTulichojifunza kutoka
kwa wapinzani ni matarajio yao makubwa ya kutumia ofi si za umma kama
sehemu ya kupora mali ya umma.
Majibu hayo ambayo yanatokana na mtazamo wa Raila kuhusiana na
uongozi wa Jubilee, yalitolewa na Kitengo cha Rais cha Mawasiliano,
ambacho ni kwa ajili ya masuala ya Rais Uhuru Kenyatta, inaonyesha kuwa
sasa vita baina ya wanasiasa hao vinapiganwa katika kiwango cha juu
kabisa.
Raila, ambaye alikuwa waziri mkuu katika utawala uliopita,
alihusishwa na kashfa ya uuzwaji wa mahindi kutoka hifadhi ya taifa na
kuwa alitoa vibali kwa familia na marafi ki zake wa karibu. Pia, na
viongozi wenzake waandamizi wamehusishwa na jinsi walivyosimamia
Programu ya Kazi kwa Vijana.
Wakati akitupiwa tuhuma hizo, Raila naye katika siku za hivi karibuni
amekuwa akiitupia shutuma za kuhusika na vitendo vya rushwa kwa
serikali iliyopo madarakani.
Mbinu mojawapo inayotumiwa na Muungano wa
Jubilee ni kama vile kujaribu kukata miguu ya kiongozi huyo kwa kuibua
hoja ambazo zilikuwa na utata.

0 comments:
Post a Comment