Thursday, January 14, 2016

Mkuu Mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro afanya ziara manispaa ya Moshi kwa kukagua ujenzi mradi wa Maji utakaohudumia watu 9000 wa kata ya Languo,
Rau na kuboroloni na kuagiza kasi ya ujenzi iongezwe . Mradi unagharimu Fedha sh 675m
Amezindua Maabara Shule ya sekondari ya Anna Mkapa na kuutaka viongozi wa manispaa kupitia mapato ya ndani kukamilisha vifaa vilivyobaki
Aidha katika kikao cha majumuisho Kamati ya Ulinzi ya wilaya, madiwani, waratibu wa Elimu Kata na watendaji wa kata ametoa maelekezo yafuatayo
1. Mkoa wa kilimanjaro ktk Matokeo ya darasa la saba umeshika nafasi ya 4 kitaifa. Ameagiza watoto wote waliofaulu waende Shule na watoro wote wasakwe. Elimu ni bure na Fedha za kutoa Elimu bure mkoa umepokea sh 998,935,000. Ameagiza wakuu wa Shule kutumia Fedha hizo kwa uangalifu
2.Ameagiza kila halmashauri kupanda miti milioni moja ili kurejesha mkoa kilimanjaro katika mazingira mazuri, amepiga marufuku uchafuzi wa mazingira na kuharibifu wa vyanzo vya Maji na wote waliojenga na kufanya shughuli za kijamii ktk vyanzo vya Maji kwa mujibu wa sheria ya mazingira waondoke mara moja
3. Ameagiza wote waliojitwalia maeneo ya wazi wararudishe mara moja amehaidi kupambana na wote wenye tamaa ya kujitwalia maeneo ya wazi ikiwemo viwanja vya Shule
4.Amepiga marufuku uchomaji wa matofali katikati ya jamii na kusababisha madhara











0 comments:

Post a Comment