Posted by Williammalecela.com on Monday, January 25, 2016
 |
Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh. Amos Makalla wilayani Mwanga leo Ameweka jiwe la
msingi ujenzi wa hostel ya wasichana sekondari ya Mandaka, uzinduzi
studio baadaye itakuwa Redio na television itwayo KIMS tv and Redio
station na ujenzi wa dampo Katika kikao cha watendaji wa vijijini, kata , tarafa, madiwani na Kamati ya Ulinzi na usalama ameelekeza yafuatayo
1. Amekemea tabia ya kuuza ardhi kiholela vijijini bila kufuata
utaratibu. Mahitaji ya ardhi yanaongezeka lakini ardhi haiongekezki
hivyo tuwe makini 2. Ameiagiza Kamati za maafa wilaya zote
kujipanga kufuatia taarifa toka Mamlaka ya hali ya hewa kuhusu mvua
Nyingi zinazotarajiwa kunyesha hivyo wananchi wote wanapaswa wachukue
tahadhari 3.Ameagiza halmashauri zote kuwa na dampo za kisasa kwani
suala la usafi ni ajenda ya kudumu na takataka zisombwe kwa wakati na
zitupwe kwenye dampo rasmi siyo porini au makorongoni |
0 comments:
Post a Comment