Saturday, January 2, 2016

KIDOA (4) 
Video Queen maarufu Bongo, Asha Salum ‘Kidoa’.
Video Queen maarufu Bongo, Asha Salum ‘Kidoa’ amemtangazia vita mpenzi wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’ akidai atafanya kila njia amnase msanii huyo.
Rafiki wa karibu wa Kidoa aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini alidai kuwa, Kidoa alikuwa akimpenda sana Diamond hata kabla ya kuwa na Zari ndiyo maana ana ndoto za kuwa naye.
ZARI47817 Mpenzi wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’.
“Kidoa anamzimia sana Diamond, achilia mbali kumpenda kutokana na kazi yake ya muziki lakini pia kimapenzi, maana kuna wakati anakosa raha kabisa anapowaona Zari na Diamond wakiwa kimahaba,” anadai mtoa habari huyo.

0 comments:

Post a Comment