Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ichunguze iwapo kuna wizi unaofanywa na kampuni za simu kwa wateja wake.
Ngonyani alitoa maagizo hayo jana katika hafla ya uzinduzi wa duka la ‘Airtel EXPO’ linalotoa huduma mbalimbali za simu na elimu ya matumizi ya vifaa vya mawasiliano akisema amepokea malalamiko ya aina mbili kutoka kwa Watanzania wanaotumia huduma za kampuni za simu nchini.
Ngonyani alisema kutokana na mazingira hayo, imekuwa ikijengeka taswira kwamba, watumishi wa kampuni za simu wanahusika katika wizi huo. Aliiagiza TCRA kuchunguza tuhuma hizo huku akiwataka wananchi kuwasilisha malalamiko yao katika mamlaka hayo ili kutafuta ufumbuzi.
Kwa mujibu TCRA, Watanzania milioni 32 wanatumia huduma simu za mkononi, sawa na asilimia 67 huku takriban wateja milioni nane wakitumia za intaneti.

0 comments:
Post a Comment