Tuesday, January 26, 2016




RAIS John Magufuli amempongeza Rais mstaafu, Jakaya Kikwete kwa kuteuliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon kuunda jopo la watu mashuhuri.

Watu hao watamshauri Kimoon juu ya namna bora ya kuendeleza na kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu, hususan katika afya ya uzazi ya mama na mtoto.

Hayo yamo kwenye taarifa kwa vyombo vya habari, iliyotolewa na Kurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, jijini Dar es Salaam jana.

Ilisema jopo hilo la watu mashuhuri, linaongozwa na wenyeviti wenza, Rais wa Chile, Michelle Bachelet na Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Desalegn.

Rais mstaafu Kikwete na Rais mstaafu wa Finland, Tarja Halonen wameteuliwa kuwa wenyeviti mbadala.
“Kuteuliwa kwa Rais Kikwete kuwa miongoni mwa jopo la kumshauri Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kumeijengea heshima Tanzania na kumechochea matumaini ya mafanikio ya kukabiliana na changamoto za afya ya mama na mtoto, hususan kwa nchi zinazoendelea, ikiwemo Tanzania,” ilisema taarifa hiyo ya Ikulu.

0 comments:

Post a Comment