Sunday, January 3, 2016





Serikali imeiagiza kampuni ya JOYTI STRUCTURE inayosimika nguzo za mradi mkubwa wa umeme kutoka Iringa mpaka Shinyanga katika eneo la Dodoma Singida kuhakikisha anakamilisha kazi hiyo ifikapo tarehe 20 mwezi April kama mkataba unavyoelekeza la sivyo atataifishiwa mali na kufikishwa mahakamani kufuatia kusuasua kwa utekelezaji wake ambao umefikia asilimia 30 tu mpaka sasa.

Mradi huo wa Msongo wa Kilovolt 400 maarufu kama BACK BONE wenye urefu wa zaidi ya kilometa 670 unatarajiwa kuwa mkombozi wa nishati ya umeme katika mikoa ya kanda ya kati na ziwa ambapo mkandarasi anaye simika nguzo na kutandaza nyaya katika eneo la Dodoma-Singida tayari amelipwa asilimia 65 ya fedha huku akitakiwa akabidhi kazi hiyo april 20 mwaka huu kama mkataba kati yake na serikali unavyoelekeza.
 
Naibu waziri huyo pia akatembelea eneo la kikombo ambapo kuna mgogoro kati ya Tanesco na kampuni hodhi la usimamizi wa rasilimali za reli kuhusu malipo ya kupitisha nyaya za umeme juu ya reli katika eneo hilo na kuagiza mgogoro huo kumalizwa mara moja ili wananchi wa kata hiyo waweze kupata umeme.
 
Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa maeneo mbalimbali ya Dodoma wakaomba kasi ya usambazaji wa umeme  hasa maeneo ya vijijini kupitia mradi wa REA kuongezeka ili wananchi waweze kutumia nishati hiyo kuharakisha maendeleo na kujikwamua kiuchumi.

0 comments:

Post a Comment