Serikali
imeiagiza kampuni ya JOYTI STRUCTURE inayosimika nguzo za mradi mkubwa
wa umeme kutoka Iringa mpaka Shinyanga katika eneo la Dodoma Singida
kuhakikisha anakamilisha kazi hiyo ifikapo tarehe 20 mwezi April kama
mkataba unavyoelekeza la sivyo atataifishiwa mali na kufikishwa
mahakamani kufuatia kusuasua kwa utekelezaji wake ambao umefikia
asilimia 30 tu mpaka sasa.
Mradi huo wa Msongo wa Kilovolt 400 maarufu kama BACK BONE wenye
urefu wa zaidi ya kilometa 670 unatarajiwa kuwa mkombozi wa nishati ya
umeme katika mikoa ya kanda ya kati na ziwa ambapo mkandarasi anaye
simika nguzo na kutandaza nyaya katika eneo la Dodoma-Singida tayari
amelipwa asilimia 65 ya fedha huku akitakiwa akabidhi kazi hiyo april 20
mwaka huu kama mkataba kati yake na serikali unavyoelekeza.
Naibu waziri huyo pia akatembelea eneo la kikombo ambapo kuna
mgogoro kati ya Tanesco na kampuni hodhi la usimamizi wa rasilimali za
reli kuhusu malipo ya kupitisha nyaya za umeme juu ya reli katika eneo
hilo na kuagiza mgogoro huo kumalizwa mara moja ili wananchi wa kata
hiyo waweze kupata umeme.
Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa maeneo mbalimbali ya Dodoma
wakaomba kasi ya usambazaji wa umeme hasa maeneo ya vijijini kupitia
mradi wa REA kuongezeka ili wananchi waweze kutumia nishati hiyo
kuharakisha maendeleo na kujikwamua kiuchumi.
0 comments:
Post a Comment