Sunday, January 10, 2016

 
 
 
Serikali imeelezea azma yake ya kuurejesha muswada wa huduma za vyombo vya habari Bungeni huku ikisisitiza Muswada huo utarejeshwa baada ya majadiliano  na maafikiano ya kina  na wadau.
azma hiyo ya serikali imetolewa jijini Dar es Salaam na wazairi wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Mh.Napen Nauye ambapo amesema mpango wa serikali ni kuhakikisha muswada huo unakuwa shirikishi ili kuijenga tasnia ya habari nchini.
 
Katika mkutano huo uliowashirikisha wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini, wahariri hao licha ya kupongeza azma hiyo ya serikali wamesema ni vema serikali ihahakikisha majadiliano ya upatikanaji sheria bora ya habari yanafanikiwa.
 
Mh.Nape amewahakikishia wadau wa tasnia ya habari kuwa serikali ya awamu ya tano inania thabiti ya kuurejesha muswada wa huduma za vyombo vya habari ulio na uwiano sawa kati ya seriklai na wadau hao ili kuiimarisha tasinia hiyo muhimu  ya  habari hapa nchini.
 
Mapema june 2015 serikali iliridhia kuondolewa kwa  muswada wa sheria ya haki ya kupata  habari ya ya mwaka 2015 baada ya wadau wa habari kuugomea muswada huo kwakutokukidhi matwaka ya tasnia ya habari hapa nchini.

0 comments:

Post a Comment