Sunday, January 24, 2016




SPIKA wa Bunge la Uganda, Rebecca Kadaga (Mb), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika (CWP) Kimataifa ameziasa nchi wanachama wa Sekretarieti ya CWP kuendelea kuwathamini wanawake kwa kuwapa vipaumbele vya ushiriki katika ngazi za maamuzi pamoja na kuwaenzi wanawake waliotoa mchango wa maendeleo ya nchi zao.

Spika Kadaga aliyasema hayo juzi Dar es Salaam wakati akifunga rasmi warsha ya siku mbili iliyohusu kujadili ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi ili kubuni mbinu na mikakati ya kuongeza idadi ya wanawake katika ngazi za siasa na kijamii.

Kadaga alisema nchi wanachama hazina budi kuthamini mchango mkubwa wa wanawake katika masuala ya kijamii pamoja na kisiasa, hivyo kuna haja ya kuwaenzi kwa kutunza nyaraka zao muhimu ikiwemo kuwaendeleza wanawake kielimu ili kuweza kuleta maendeleo katika nchi husika.

0 comments:

Post a Comment