Monday, January 11, 2016

3Utamaduni! Mzazi mwenzake staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari’, anadaiwa kumpeleka mwanaye Latiffah Nasibu ‘Tiffah’ (miezi 5) kijijini kwao Uganda ambako amefanyiwa tambiko la kimila huku Diamond akiichomolea mbali safari hiyo, Ijumaa Wikienda lina kitu cha kushika mkononi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, tukio hilo linalofanywa na makabila mengi ya Afrika, lilijiri Ijumaa iliyopita mjini Jinja, nchini humo na kuhudhuriwa na wana ukoo wa Zari, wakiwemo pia wajomba huku bibi Zari akiwa ndiye mwenye shughuli hiyo kwa kusaidiwa na mwanaye, bibi Tiffah ambaye pia ni mama mzazi wa Zari, Halima Hassan.  

1 comment:

  1. Hahaha Tanzanian newpapers are the winner in exaggerating things.That's matooke in banana leaves ati goat's meat.Did u see the goat being slaughtered? Actually there is no such custom amongst the basoga.

    ReplyDelete