Sunday, January 3, 2016

Baadhi ya wajumbe wa Timu ya kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi ,Wizara ya maji, na umwagiliaji , Shirika l Umeme Tanzania (Tanesco )pamoja na Watalamu wa bonde la mto Rufiji wakipata maelezo ya namna ambavyo umeme wa maji huzalishwa katika kituo cha Kihansi .

Timu ya wataalam  kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Wizara ya kilimo, mifugo na Uvuvi ,Wizara ya maji, na Umwagiliaji , Shirika l Umeme Tanzania (Tanesco ) pamoja na Watalamu wa bonde la mto Rufiji waliotembelea  vyanzo vya maji vinavyotiririsha  maji katika mito inayomwaga maji  mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji ikiwemo  Mtera, Kihansi na Kidatu ili kuunganisha nguvu ya pamoja na kurejesha vyanzo hivyo katika hali yake ya awali kutokana na kuathiriwa na shughuli za kibinadamu na hivyo kusababisha kukauka na upungufu wa maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji ilivyokuwa katika miaka ya nyuma.
 Muonekano wa Bwawa la Kihansi kwa sasa ambalo pia limepunguza uzalishaji wa umeme wa maji kutokana na kupungua kwa kina cha maji.
 Timu ya wataalamu  kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi ,Wizara ya maji, na umwagiliaji , Shirika l Umeme Tanzania (Tanesco )pamoja na Watalamu wa bonde la mto Rufiji waliotembelea  vyanzo vya maji vinavyotiririsha  maji katika Mabwawa ya kuzalisha umeme .
 Eneo lenye  chanzo cha cha maji pamoja na mto  mbalo hutumiwa kwa shughuli za kibinadamu na kusababisha upotevu wa maji yanayoingia katika mto unaomwaga maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji
 Moja ya sehemu ya mashine ama mtambo inayotumika kuzalisha umeme wa maji katika vituo vya Kihansi, Kitadu na Mtera.
 Mashine inayotumika kuondoa  taka  kama vile magogo na nyingine zanamna hiyo katika mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji.

0 comments:

Post a Comment