Sunday, February 7, 2016


 

Maswali mengi yameibuka hivi karibuni baada ya wadau mbalimbali wa masuala ya siasa kutolisikia jina la mbunge wa kigoma mjini Zitto Kabwe kwa tiketi ya ACT Wazalendo likitajwa na mwenyekiti wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Freeman Mbowe katika baraza la mawaziri vivuli.

Kiongozi wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Freeman Mbowe jana alitangaza orodha ya majina ya wabunge wa upinzani wanaounda baraza la mawaziri vivuli, huku akimtosa Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe.

Maswali mengi yaliibuka na kuzua mjadala kwanini Mbowe ameamua kumuacha Zitto haliyakuwa hivi karibuni wameshirikiana vyema katika kupinga hoja za serikali ikiwemo ile ya kutooneshwa LIVE kwa vipindi vya Bunge katika luninga ya Taifa TBC, na kutoka na tamko moja kama wapinzani.

“Ukawa tulisaini tamko la pamoja la ushirikiano na hiyo ilikuwa katika Bunge la Katiba. Kumbuka tumeshirikiana katika Uchaguzi Mkuu na kupata madiwani na wabunge ambao ndiyo hawa wamezaa baraza hili,”

“Ushirikiano wetu upo katika halmashauri na majiji. Kutokana na jambo hilo huwezi kuiingiza ACT maana haikuwapo katika makubaliano ya Ukawa,”

0 comments:

Post a Comment