Sunday, February 28, 2016

 
Mungu ni mwema! Leo kama ada tunakutana mpenzi msomaji wangu wa Love & Life katika kilinge chetu hiki kwa lengo la kuelimishana na kukumbushana masuala ya mahusiano ambayo yametawala kwa kiasi kikubwa maisha yetu.Leo tutazungumzia kuhusu tatizo linaloonekana kukithiri na kuwatatiza watu wengi ambao wamejaribu kuingia kwenye uhusiano wa mapenzi na kujikuta wakiambulia maumivu ya kuachwa kila mara na watu waliowakabidhi mioyo yao wakiamini wataishi pamoja mpaka kifo kuwatenganisha.

Tukubaliane kwamba, kutendwa au kuachwa kwenye mapenzi ni jambo la kawaida. Watu wengi wamewahi kuachwa na wapenzi wao na katika hali nyingine watu haohao waliotendwa huweza kuwaacha wapenzi wengine waliowapenda; yote hii ni kawaida, lakini hali hii huwa tatizo pale ambapo mtu anayeachwa au kuumizwa anakuwa ni yuleyule. 

0 comments:

Post a Comment