
Msanii wa muziki, Barakah Da Prince amewapa za uso watu wanaomchafua kwa kusema kuwa wana mahusiano nae, na kusema jitihada zao za kumuharibia taswira yake kwenye jamii zimegonga mwamba.
Kupitia instagram, Barakah amepost picha na kuandika.
My life na huyu tu ndio namtambua, hao mnawatambua ninyi, haya ni maisha yangu,na yapo kwenye serekali yangu, usitake niishi unavyotaka, mnajaribu sana kuchafua jina langu kwa mashabiki zangu, na pia mnajarbu kushusha heshima yangu kwa wanaonieshimu ila mmechelewa sana, nachoamini shabiki wa kweli awezi nichukia kwa upumbavu au uvumi wa kijinga unaoendelea, hii ya mtoto imegoma tengenezi nyingine tena,na tambueni haya ni maisha yangu #SUPER na tumeshamjua anaewatuma kunichafua.
Baraka hivi karibuni alikanusha kuwa na mahusiano na msanii wa filamu za kibongo Nisher ambaye alikuwa anasema kuwa ni mpenzi wake.
0 comments:
Post a Comment