Siku ya March 11 2016 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda alifanya ziara ya kutembelea katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Kinondoni kujionea kero za uharibifu wa miundombinu ikiwepo barabara na kuamua kutoa agizo kwa Manispaa ya hiyo kuhakikisha inafanya ukarabati wa maeneo yaliyoharibika ndani ya siku 14 kabla ya kuwawajibisha.
Leo March 25 ripota wa millardayo.com aliongozana na mkuu huyo wa mkoa katika mitaa tofauti ikiwa ni pamoja na barabara ya Mwananyamala ili kujionea hatua zilizofikiwa na kukuta ukarabati ukiendelea…
Barabara ya kutokea Makumbusho kuelekea Mwananyamala
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda wakati akikagua barabara
Hiki ni kipande cha barabara ambacho bado hakijafanyiwa marekebisho
Wafanyakazi wakiendelea kupiga kazi
Hapa huruhusiwi kupita wakati ujenzi ukiendelea
Jamaa kataka kupenya wakamrudisha alipotoka
Watu wakipiga kazi
Jamaa akizibua moja ya mtaro ulioziba kwa uchafu
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akicheki maendeleo
Barabara ya Mwananyamala sokoni
Barabara imefungwa ili kuzuia watu wasipite kuharibu utaratibu wa kazi
Mifereji pia imesafishwa kuondoa uchafu
Baada ya kuhakikisha kazi inaenda, mkuu wa mkoa na watu wake wakipiga stori
0 comments:
Post a Comment