March 5 2016 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda alitembelea katika shule ya sekondari Turiani, Dar es salaam kwa lengo la kuzindua vitambulisho vitakavyotumika na Walimu wa Dar kwaajili ya kupanda daladala bure kuanzia March 7 2016.
Hii inakuja siku baada ya Dc Makonda na Wamiliki wa usafiri wa daladala jiji la Dar es salaam kukubaliana kuanza kutoa huduma hiyo ya usafiri wa bure kwa Walimu, lakini katika hali hiyo, kuna baadhi ya watu wamekuwa na maoni tofauti kuhusu huduma hiyo huku wengine wakidiliki hata kuupinga mchakato huo, hapa Mkuu wa wa Wilaya Dc Makonda anasema>> ‘Ndoto yanguninatamani kila iitwapo leo Mwalimu akiingia barabarani kila mtu anaweka heshima, watu wasio na fikra pana wao kazi yao ni kulaumutu bila sababu ‘
Unaweza kuitazama hapa Full video ya Dc Makonda na Walimu…..

0 comments:
Post a Comment