Don ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na EATV katika kipindi cha E News ambapo amesema kwamba msanii huyo ana nafasi kubwa ya kufanya vizuri kutokana na mabadiliko chanya ambayo yanaonekana kwa hivi sasa.
”Nilikuwa ‘inspired’ sana kutengeneza ngoma na Ray C kwa hiyo tulipokubaliana kufanya hivyo nimeamua kujitolea kutengeneza wimbo huo”-Amesema Don
Kuhusu suala la Ray C kurudia kutumia madawa ya kulevya Don amesema hajawahi kumwona akifanya hivyo na kwa hali aliyonayo kwa sasa hatumii tena madawa hayo kama anavyozushiwa na baadhi ya watu.
0 comments:
Post a Comment