Wednesday, March 30, 2016


@Le Mutuz Nation Straight Talk!!:- Narudia tena Binadam hafanikiwi kwa kutegemea misaada, MCC wanaweza kubaki na misaada yao Tanzania tutaendelea kuongozwa kama wao USA kwa kutumia Sheria sio Misaada, Maalim Seifu kama alidhulumiwa kwenye uchaguzi alitakiwa kwenda Mahakamani sio MCC, Al-Gore mgombea urais wa USA walipomuibia kura alienda Mahakamani hakuenda China kushitaki Serikali ya USA ifutiwe mikopo!!.....Kuna Wabongo wenzetu kwa kukosa hoja za kushindana na Serikali ya Magufuli wameamua kulibebea bango hili jambo la kitoto sana, ila ni hao hao siku za nyuma walituambia CUF ni chama cha mashoga walipowahitaji wakajiunga nao, baadaye wakasema Lowassa ni Shetani walipohitaji pesa zake wakasema ni Malaika, hao hao walituambia hatuhitaji hela za MCC leo hao hao wanasema tunazihitaji sana!!
- Masikini wa Mungu huwa wanaimbishwa tu nyimbo na Viongozi wao bila hata kuuliza mtungaji ni nani, hahahaha wamesahau kwamba kina Mobuttu, Savimbi na Saddam Hussein waliwahi kuimba nyimbo kama zao USA ilipomaliza kazi nao wakawaua, akili ya kushikiwa na changanya na yako sometimes sio kila kitu lazima uamuliwe na form six. Zanzibar ni nchi huru yenye Sheria zake ambazo kama za USA zinataka mtu aliyenyimwa haki zake kwenda mahakamani sio kwenda nje ya nchi kulilia misaada ikatwe ili haki yake ipatikane, poleni sana wapinzani ila Tanzania tutakuwa wendawazimu kukubali kuburuzwa kwa sababu ya misaada, TO HELL WITH MCC!! - le Mutuz Nation

0 comments:

Post a Comment