MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa
Tanzania, Mbwana Ally Samatta
ametokea benchi na kuifungia timu
yake, KRC Genk katika ushindi wa
4-0 dhidi ya KV Oostende kwenye
mchezo wa Ligi Ku ya Ubelgiji
usiku huu.
Katika mchezo huo uliofanyika
Uwanja wa Cristal Arena, mjini Genk,
Nahodha wa Tanzania, Samatta
alifunga bao hilo dakika ya 77, ikiwa
ni dakika moja tu baada ya kuingia
kuchukua nafasi ya Nikolaos Karelis.
Mabao mengine ya Genk
yamefungwa na Pozuelo dakika ya
12, T. Buffel dakika ya 21 na N.
Kebano dakika ya 85.
Hilo linakuwa bao la tatu kwa
Samatta katika mechi nane
alizocheza tangu ajiunge na Genk
Januari mwaka huu akitokea TP
Mazembe ya DRC.
Kabla ya kufunga katika ushindi wa
4-1 dhidi ya KV Oostende, Samatta
pia alifunga katika ushindi wa 3-2
baada ya kuingia dakika 15 za
mwisho dhidi ya Club Brugge.
Mechi nyingine alizocheza Samatta
tangu atue Genk, zote akitokea
benchi dakika za mwishoni ni dhidi
ya Standard Liege (Genk)
wakifungwa 2-1, dhidi ya Lokeren
wakitoa sare ya 0-0, dhidi ya
Waasland-Beveren wakishinda 6-1
na dhidi ya Mouscron-Peruwelz
wakishinda 1-0 pia ugenini na dhidi
ya Anderlecht wakifungwa 1-0.
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa
Tanzania, Mbwana Ally Samatta
ametokea benchi na kuifungia timu
yake, KRC Genk katika ushindi wa
4-0 dhidi ya KV Oostende kwenye
mchezo wa Ligi Ku ya Ubelgiji
usiku huu.
Katika mchezo huo uliofanyika
Uwanja wa Cristal Arena, mjini Genk,
Nahodha wa Tanzania, Samatta
alifunga bao hilo dakika ya 77, ikiwa
ni dakika moja tu baada ya kuingia
kuchukua nafasi ya Nikolaos Karelis.
Mabao mengine ya Genk
yamefungwa na Pozuelo dakika ya
12, T. Buffel dakika ya 21 na N.
Kebano dakika ya 85.
Hilo linakuwa bao la tatu kwa
Samatta katika mechi nane
alizocheza tangu ajiunge na Genk
Januari mwaka huu akitokea TP
Mazembe ya DRC.
Kabla ya kufunga katika ushindi wa
4-1 dhidi ya KV Oostende, Samatta
pia alifunga katika ushindi wa 3-2
baada ya kuingia dakika 15 za
mwisho dhidi ya Club Brugge.
Mechi nyingine alizocheza Samatta
tangu atue Genk, zote akitokea
benchi dakika za mwishoni ni dhidi
ya Standard Liege (Genk)
wakifungwa 2-1, dhidi ya Lokeren
wakitoa sare ya 0-0, dhidi ya
Waasland-Beveren wakishinda 6-1
na dhidi ya Mouscron-Peruwelz
wakishinda 1-0 pia ugenini na dhidi
ya Anderlecht wakifungwa 1-0.
on
0 comments:
Post a Comment