Friday, May 20, 2016

 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Akutana na kuzungumza na wenyeviti wa Vijiji, watendaji wa Vijiji na kata Halmashauri ya Kyela
Amewataka viongozi na watendaji kupitia Kamati za Ulinzi na usalama kufanya mikutano wa uelimishaji wananchi kuacha kuwaficha, kuwasaidia wahamiaji haramu kuingia nchini au kuwapitisha kwenda nchi ya jirani ya Malawi. Amewaambia usiku wa kuamkia leo wahamiaji haramu 8 wamekamatwa wilayani Kyela
Aidha amewataka kudhibiti magendo ya bidhaa zinazopitishwa kupitia njia za panya zipatazo 32. Kutodhibiti njia hizo serikali itakosa mapato lakini pia bidhaa zitakazoungizwa nchini bila kukaguliwa ni hatari kwa matumizi ya binadamu 

0 comments:

Post a Comment