Monday, June 6, 2016




Kama mzaha vile, bila kujali ukubwa wa kiingilio, Chirstian Bella anaujaza ukumbi mkubwa wa Escape One katika onyesho lake maalum la miaka yake 10 katika ‘game’ hapa Tanzania.

Escape One ikashona watu mithili ya njiti za kibiri zinavyobanana kwenye box lake huku burudani za nguvu zikishushwa bila kikomo.

Katika mambo yaliyovutia ni pamoja na Bella kumwalika bosi wake wa zamani aliyemleta hapa Bongo - Prof. Juma Kapuya (mmiliki wa Akudo Impact.


Kapuya akawa ni mmoja wa watu muhimu waliolishwa keki na Christian Bella.

Kiingilio cha onyesho hilo kilikuwa ni elfu 20 na elfu 50 kwa ma-VIP.
 Christian Bella ameandika historia mpya katika maonyesho yake
 Christian Bella akimlisha keki Prof Juma Kapuya
Hii ni nyomi iliyojazwa na Bella hapo Escape One
Ali Kiba alikuwa mmoja wa wasanii waliopamba onyesho hilo
Christian Bella ni  Balaa
Dully Sykes (kushoto) na Khamis Dacota wa Clouds TV wakifuatilia onyesho la Bella
 
Source:- Saluti

0 comments:

Post a Comment