Thursday, July 21, 2016


RIDHIWANI Kikwete ambaye pia ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM,leo hii ameweka ujumbe kwenye ukurasa wake wa kijamii ,kuhusu sakata la JPM kukabidhiwa Uenyekiti wa CCM.

Ridhiwani ambaye pia ni Mbunge,amesema kuwa anafurahi kuona siku za JPM kukabidhiwa Chama kama Mwenyekiti zimekaribuia na kumtakia kila la kheri Dr Magufuli katika wadhifa wake huo mpya

UJUMBE TOKA HOSPITALI INDIA Awali ya yote nimshukuru Mungu kwa kuendelea kutupa uhai na uzima.ijapokuwa sisi wengine tupo mbali huku.tukitafuta tiba. Kwa sie tunaoamini Mungu tunajua kuugua ni sehemu ya ibada. Inshaallah sote tulio ktk ibada hyo Mungu atuafu. J.mosi hii CCM inaingia ktk historia mpya ya kumpata mwenyekiti wake wa tano tokea kilipoundwa ,si mwingine bali ni Rais wetu wa sasa wa Jamhuri Mh John Magufuli. Rais Magufuli ameshaonyesha uwezo mkubwa wa kuongoza ktk muda mfupi wa urais wake.hvyo wanaccm kote nchini tuna matumaini makubwa na uenyekiti wake. Tunachokitaraji ni kile anachokifanya serekalini tutakiona ndani ya chama chetu. Sio siri ndani ya chama kuna uozo mwingi sana.uozo huu kwa sasa haupaswi tena kuvumiliwa kwa namna yoyote ile.Nani asiyejua ndani ya chama kuna watendaji hata kuandika tu barua ni mgogoro?halaf pia ni mchwa waliokubuhu? Huku pia tukiwa na viongozi miungu watu hasa kipindi cha chaguzi. Viongozi hawa kazi yao ni kudhulumu haki za wagombea kwa kuwakata watu wenye uwezo na kuwachukua mapoyoyo kisa ni mzigo. Pia baadhi yao wameigeuza miradi ya chama mali zao bnafsi.leo ccm miradi mingi haijulikani pesa zake zinaishia wapi!!mchwa wanajitafunia tu.Sasa kiboko yao anakabidhiwa chama j.mosi. Binafsi nnaaamini mzee Magufuli atakuja kuziba mianya hii ya kipumbavu. Sambamba na hayo kuna usaliti mkubwa sana tuliouona hususan ktk uchaguzi mkuu uliopita.kuna baadhi ya viongozi mchana walikuwa ccm usiku walikuwa ukawa.hawa mzee Magufuli tuondolee kabisa. Dhambi ya usaliti ndani ya chama ni kubwa na adhabu yake ni kufukuzwa tu.hatutarajii kuona wasaliti wakiendelea kuwepo tena.huku wengine wakipeperusha bendera za kijani kwenye magari yao.waende tu kwa kaka yao waliyeamini atakuwa Rais. Mm sina tatizo na wale waliokuwa na kundi wakati wa mchakato,tatizo ni wale ambao hata baada ya mchakato wa kura za maoni waliendeleza makundi. Hawa ni wasaliti na hawatufai. Nitumie fursa hii pia kums
A photo posted by Ridhiwani Kikwete (@ridhiwani_kikwete) on

0 comments:

Post a Comment