Saturday, July 23, 2016

MASOGANGE5
Mjini hakukaliki! Mkakati wa Rais Dk. John Pombe Magufuli ‘JPM’ wa kupambana na biashara haramu ya dawa za kulevya ‘unga’ hapa nchini, umeiva ambapo uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba unawatumia baadhi ya mastaa Bongo kuwakamata vigogo wanaojihusisha na biashara hiyo.

WAANZIA KWA ‘MATEJA’ Uchunguzi huo wa wiki kadhaa jijini Dar ulibaini kwamba mara tu baada ya Rais Magufuli kutangaza kupambana na mfumo wa wauza unga, kikosi maalum cha Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Maofisa wa Uhamiaji waliingia kazini ‘fasta’ ambapo walianza kwa kuwatumia watu wa chini kabisa, kuanzia kwa watumiaji wa unga (mateja) ili kupata mwanga wa wapi wanapopata dawa hizo.

0 comments:

Post a Comment