Friday, August 5, 2016

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Amos Makalla leo,
- Akagua miradi 6 ya MAJI halmashauri Mbeya
- Wakandarasi 5 kati YA 6 wametelekeza miradi YA MAJI
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla ametoa siku saba wakandarasi wa miradi ya MAJI Mkoa wa Mbeya kurudi haraka kukamilisha miradi waliyoitelekeza kwa kisingizio cha madai ya Fedha
Ametoa agizo hilo leo katka ziara ya kukagua miradi 6 ya MAJI inayolenga kuhudumia Vijiji 17 na kukuta miradi hiyo imetelekezwa na wakandarasi na kufifisha matumaini ya wananchi kupata huduma ya MAJI
Ameagiza wakandarasi hao kurudi na kuwasilisha certificates za madai yao kwa ajili ya malipo na ametangaza kuwa wizara ya MAJI kwasasa haiwezi kuleta Fedha mpaka wapate madai ili waweze kulipa
Amesema ameshangaa na amehaidi kuchukua hatua baada ya kugundua baadhi ya miradi wakandarasi wamelipwa Fedha Nyingi kuliko kazi zilizofanyika na amesema aina ya wakandarasi hao wakikaidi kurudi watakamatwa
Aidha amewataka wananchi na viongozi wa maeneo miradi hii inayotekelezwa wasioikee miradi yenye dosari na ameagiza halmashauri kutokulipa Fedha zote moaka muda wa miezi sita ya uangalizi wa mradi.










0 comments:

Post a Comment